Watatu wa familia moja wafukiwa na kifusi

Friday, January 15, 2010 / Posted by ishak /

WATU watatu wa familia moja wamekufa kufuatiwa kufukiwa na kifusi na mwingine kusombwa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Arusha



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Basilio Matei, amethibitisha matukio hayo na kusema vifo vya watu hao vimetokana na kufukiwa na vifusi na kuswombwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika wilaya za Longido na Arumeru mkoani humo.

Alisema mwili wa mtu mmoja uliokotwa ukiwa na majeraha unaosadikiwa kuwa kifo chake kilitokana na mvua hizo.

Kamanda Matei alisema watatu wengine wa familia moja walikutwa katika machimbo ya Moramu Mweupe wa Kujengea Nyumba, baba na watoto walikutwa wamekufa kufuatiwa kufumikwa na kifusi kilichosombwa na mvua na kuwafunuka.

Mvua hizo zimekuwa zikiathiri watu wengi katika mikoa tofauti tofauti na kusababisha vifo na nyumba kubomoka katika sehemu tofauti nchini

Kutuatia mvua hizo wilayani Kilosa mkoani Morogoro, wilaya hiyo imeendelea kukumbwa na mafuriko kufuatia mvua zinazonyesha hivi sasa ambapo katika kitongoji cha Mateteni, Kijiji cha Mbiligili, jumla kaya 173 zenye watu 225 nyumba zao zimezungukwa na maji.

Hivi sasa watu hao wamehifadhiwa katika kambi iliyokuwa ya wakimbizi eneo la Shule ya Msingi Dakawa Centre baada ya kukumbwa na mafuriko na nyumba zao kuzingirwa na maji.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Halima Dendegu, alisema mafuriko hayo yalianza kutokea usiku wa kuamkia Januari 12, mwaka huu baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha mto Mkundi kujaa maji na kusambaa katika vijiji vilivyo jirani na mto huo.

0 comments:

Post a Comment