
Rais wa Nigeria, Alhaji Umaru Yar'Adua ambaye kiti chake cha urais kimekuwa kikikaliwa na makamu wake kwa miezi kadhaa sasa baada ya rais huyo kuugua ugonjwa wa moyo, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 58.
Kwa mujibu wa msemaji wa rais huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake wakati akiongea na shirika la habari la BBC, alisema kwamba rais Yar'Adua amefariki dunia jana jumatano ingawa serikali ya Nigeria bado haijatoa taarifa rasmi.
Rais Yar'Adua alichaguliwa kuwa rais mwaka 2007 lakini kutokana na matatizo ya moyo na figo hajaonekana kwa wananchi wake kwa miezi kadhaa.
Baada ya rais huyo kuugua muda mrefu huku akipatiwa matibabu nchini Saudi Arabia, hatimaye makamu wa rais, Goodluck Jonathan aliteuliwa kushikilia nafasi yake mpaka rais huyo atakapopona.
Taarifa zinasema kuwa rais huyo aliiaga dunia jana jumatano kwenye villa lake nchini Nigeria kwenye majira ya kati ya saa tatu na saa nne usiku kwa saa za Tanzania.
Yar'Adua alienda Jeddah, Saudi Arabia kwaajili ya matibabu mwezi Novemba mwaka jana na alitumia miezi mingi sana huko kiasi cha wapinzani wake na viongozi wa zamani wa Nigeria kumshauri ajiuzulu.
Wakati huo Yar'Adua alimkabidhi mikoba ya urais makamu wake, Goodluck Jonathan lakini hata aliporudi toka Saudi Arabia mwezi februari mwaka huu, Goodluck Jonathan aliendelea kukikalia kiti cha urais.
Taarifa zinasema kuwa baada ya kufariki kwa rais Yar'Adua, makamu wake wa rais ataapishwa rasmi kuwa rais katika siku zijazo.
source nifahamishe
Ile fainali ya mchezo wa kiduku ambao wanaume huvaa nguo za kike wakishindana kukatika mauno kama wanawake imefanyika na muaandaji wa mashindano hayo amepongezwa kwa kuwaletea wabongo ubunifu mpya ingawa baadhi ya wadau wanahofia mchezo huo utawaharibu vijana.
Ilikuwa ni usiku ambao kusema kweli nilisikitika kumuona mwanaume akiwa amevaa sidiria na gagulo akikatika viuno kama mwanamke.
Kijana mwingine naye bila haya aliyabenua makalio yake kumuelekezea mwenzake huku akikata mauno ambayo yalinifanya nijiulize wapi tunawapeleka vijana wa taifa la kesho.
Hiyo ilikuwa ni sehemu ya vionjo vya fainali ya kiduku ambapo vijana wa kitanzania walishindana kukata mauno kuwania dola 250.
Katika fainali hiyo kundi la Visqua toka kiwalani ndilo lililowashinda wenzao kwa mauno na kutunukiwa dola 250.
Mamia ya watu walifurika kwenye ukumbi wa Travertine, Magomeni kushuhudia fainali hizo.
Ingawa baadhi ya wadau wanauona mchezo wa kiduku kama vile unawahatarisha vijana kugeuka kuwa mashoga, muandaaji wa mashindano hayo Maimartha wa Jesse alipongezwa sana na kusifiwa kwa ubunifu wake wa kutuletea watanzania mchezo mpya aliouita kiduku.
Wiki mbili zilizopita niliwaletea picha za hatua ya awali ya mashindano ya Kiduku na wadau wengi walikasirishwa na wanafunzi wakiwa katika unifomu za shule kushiriki kwenye mashindano hayo.
Vijana wengine walionekana wakiwa wamevaa vipande viwili vya kanga hali iliyowafanya watu wengi waweke maswali ya kuuliza muandaaji wa kiduku ana malengo gani.
Hata hivyo Mgeni rasmi wa fainali za kiduku zilizofanyika jumamosi alikuwa mbunge wa Kinondoni, Mh. Iddi Azzan wakati viongozi wa klabu ya Simba walikuwa wageni waalikwa na walikuja na kombe lao la ligi kuu ya bara walilolitwaa wiki chache zilizopita.
source nifahamishe
Maiti za Watu Kuuzwa Kwenye Supermarket Ujerumani

Yule daktari bingwa wa mifupa wa Ujerumani ambaye mwaka jana aliandaa maonyesho ya maiti zikifanya mapenzi, ameamua kufungua supermarket ambapo atauza vipande vya miili ya watu.
Baada ya kuandaa maonyesho mwaka jana akizionyesha maiti katika hali mbalimbali za kujamiiana, Dr. Gunther von Hagens wa nchini Ujerumani ameamua kuwauzia watu maiti za watu alizo nazo.
Hagens anafungua supermarket ya maiti za binadamu mjini Guben, Brandenburg, ambayo imepangwa kufunguliwa rasmi mei 28 mwaka huu.
Fuvu la binadamu likiwa limening'inizwa kwenye chuma litauzwa euro 1,200.
Hagens pia ana mpango wa kufungua tovuti ya duka hilo ili aweze pia kufanya mauzo online.
Hagens ambaye anajulikana zaidi kama "Dr Death" (Dokta Kifo), ni mtaalamu maarufu wa elimu ya mwili na viungo vya binadamu na wanyama (Anatomy).
Hagens anatumia njia aliyoigundua yeye mwenyewe inayojulikana kitaalamu kama "plastination" ambapo maiti hutolewa ngozi yote na kisha majimaji yote kwenye maiti kukaushwa.
Hagens hutumia plastiki zilizotengenezwa kwa madini ya silicon kuziweka maiti hizo katika maumbile mbali mbali kuonyesha maisha ya kila siku ya mwanadamu.
Hagens alisema kuwa maiti anazozitumia kwenye kazi zake ni za watu waliojitolea miili yao kwake kabla hawajafariki. Hagens aliongeza zaidi kuwa yeye mwenyewe ameishajitolea maiti yake itumike namna hiyo akishafariki.
Mwaka jana Hagens aliingia kwenye mzozo mkubwa wakati alipofungua maonyesho mjini Berlin akiyaweka maumbile ya maiti katika staili mbalimbali za kujamiiana.
Miaka miwili iliyopita Hagens alijaribu kufungua duka la kuuza vipande vya miili ya watu lakini alilazimika kuahirisha mpango wake kutokana na upinzani mkubwa toka kwa makanisa na watu mbalimbali.
Safari hii Hagens amesema ameweka nia ya kweli ya kufungua supermarket hiyo ya maiti za binadamu na amesema hatauahirisha mpango wake kwa sababu yoyote ile.
source nifahamishe
Amuua Mpenzi Wake Kwa Staili ya Ajabu ya Mapenzi

Mwanaume mmoja nchini Uingereza amejikuta akipandishwa kizimbani kwa kosa la kumuua mpenzi wake wakati wakifanya mapenzi.
Vionjo katika malavidavi havikumuendea vizuri bwana Jason O'Malley, 39, ambaye amefikishwa mahakamani kwa kosa la kumuua mpenzi wake.
Jason ambaye alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanawake watatu tofauti kwa wakati mmoja, aliiambia mahakama kuwa mpenzi wake Kerry Sneddon alikuwa akimtaka awe anaikandamiza shingo yake kwa nguvu wakati wa kupeana uroda.
Jason aliwaambia maafisa wa polisi alipotiwa mbaroni kuwa ingawa alikuwa hapendi, alifuata maagizo ya mpenzi wake ya kumkaba koo kwa nguvu wakati wa kufanya mapenzi.
Jason aliongeza kuwa walishawahi kufanya hivyo mara sita au saba kabla ya siku ya tukio la kufariki kwa mpenzi wake.
Mwili wa bi Sneddon ulikutwa ukiwa hauna nguo kwenye sakafu. Shingo yake ilionyesha kuwa alikabwa koo kwa kutumia waya.
Jason aliwaambia polisi kuwa anakumbuka jinsi walivyoanza kufanya mapenzi lakini hakumbuki kitu kilichopelekea kufariki kwa mpenzi wake. Jason aliongeza kuwa hawakuwahi kutumia waya kabla ya siku hiyo.
Jason alikanusha kumuua mpenzi wake huyo ambaye alifahamiana naye kupitia mitandao ya internet ya kutafuta wachumba. Hata hivyo upande wa mashtaka umeukataa utetezi wa Jason ukisema kuwa Jason alimuua mpenzi wake baada ya kutokea marumbano kati yao.
"Mtuhumiwa alimuua Kerry Sneddon, hatukubali kuwa hii ni ajali, alitumia waya kumkaba koo na alitumia nguvu nyingi sana akiwa na nia ya kumuua au kumdhuru", mwendesha mashtaka aliiambia mahakama.
Mahakama iliambiwa kuwa Jason alikuwa na wivu sana akichungulia kila meseji iliyokuwa ikiingia kwenye simu ya bi Sneddon na pia akitaka kujua kila sehemu anayoenda.
Jason alianza kuishi na bi Sneddon mwaka 2007 baada ya kumtelekeza mkewe.
Uchunguzi wa kesi hiyo unaendelea.
source nifahamishe
SERIKALI imewataka wanafunzi wa Tanzania wanaosoma nje kufuata maagizo ya serikali yanayowazuia kutembea usiku wanapokuwa ughaibuni na kama ikilazimika kufanya hivyo, basi watembee kwa makundi.
Kauli hiyo ya serikali imetolewa bungeni jana wakati wa kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mji Mkongwe, Ibrahim Muhammad Sanya (CUF) aliyetaka kujua serikali inachukua hatua gani kwa vifo vya wanafunzi wanaosoma nchi za nje.
Akitoa kauli hiyo baada ya kujibu swali la Msingi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba kuwa pamoja katika safari hizo za usiku kama ikibidi zitaweza kusaidia katika kutoa ushahidi wa nini kilitokea na kusababisha maafa.
Katika swali lake la msingi, Sanya alitaka kujua taarifa ya kifo cha mwanafunzi aliyeuawa huko Bangalore, India hivi karibuni, Imran Mtui na kama serikali ya India imetoa kauli yoyote.
Akijibu swali hilo, alisema India kupitia kwa mkuu wake wa jeshi la polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika wataieleza serikali ya Tanzania nini kilichojiri.
Hata hivyo, taarifa za awali zilisema kwamba marehemu Mtui alikutwa kandokando ya reli, majira ya saa tatu asubuhi ya Januari 31 mwaka huu akiwa na majeraha makubwa kichwani.
Aidha, taarifa za madaktari wa India zilibaini kwamba, alikufa kutokana na mshituko na kuvuja damu kulikosababishwa na kusagwa kichwa na treni.
Alisema pia ni vigumu kuelewa mambo na kwamba kijana huyo aliyekuwa na kawaida ya kutoka na pikipiki siku hiyo alitoka bila pikipiki.
Aidha, Balozi Iddi alizungumzia mauaji ya Watanzania wanafunzi huko Marekani na kusema, uchunguzi bado unaendelea na ukimalizika pia serikali ya Marekani imesema itatoa taarifa kwa serikali ya Tanzania.
source habarileo
Wanawake Wanaovaa Vimini Ndio Wanaotuletea Mabalaa Duniani'

Mmoja wa viongozi wa juu wa kidini nchini Iran amesema kuwa wanawake wanaovaa vimini na nguo za kuwadatisha wanaume ndio chanzo cha mabalaa mbali mbali yanayotokea siku hizi kama vile matetemeko ya ardhi na tsunami.
Wanawake wanaovaa nguo zisizo za heshima zinazoyaacha wazi maungo yao wamedaiwa kuwa ndio chanzo cha mabalaa mbali mbali yanayoua maelfu ya watu ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika miaka ya hivi karibuni.
Akiongea katika sala ya ijumaa mjini Tehran nchini Iran wiki iliyopita, mmoja wa viongozi wa juu wa kidini wa Iran, Ayatollah Kazem Sedighi alisema "Wanawake wengi siku hizi hawavai nguo za heshima na matokeo yake wanawachanganya wanaume na kupelekea kuongezeka kwa matendo ya zinaa ambayo ndiyo yanayosababisha matetemeko ya ardhi na mabalaa duniani".
"Majanga yanayotokea duniani yanatokana na madhambi ya watu", aliongeza Ayatollah Sedighi.
"Hatuna njia ya kuepuka kufunikwa na vifusi vya majengo yetu zaidi ya kumrudia mungu na kufuata misingi ya dini yake ya kiislamu", aliendelea kusema Ayatollah Sedighi.
Wanawake nchini Iran hutakiwa kuvaa kwa mujibu ya misingi ya mafundisho ya kiislamu lakini wanawake wengi wamekuwa wakivunja sheria na kuacha wazi sehemu za mbele za nywele zao na pia wengine huvaa nguo zinazobana na kuonyesha maungo yao.
Iran ni miongoni mwa nchi chache duniani zinazosumbuliwa na matetemeko makubwa ya ardhi mara kwa mara.
Mwaka 2003 tetemeko kubwa la ardhi liliukumba mji wa Bam kusini mwa Iran na kuteketeza maisha ya watu 31,000.
Mwanzoni mwa mwezi huu, rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, aliwaonya wakazi milioni tano wa mji mkuu wa Iran, Tehran kuwa waukimbie mji huo kwani tetemeko kubwa la ardhi huenda likatokea wakati wowote.
source nifahamishe
'ChemChem' ya Pesa Mkoani Ruvuma Yavuta Wengi
WAKAZI wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wamekuwa wakikesha wilayani humo usiku na mchana wakisubiria pesa zinazotoka chini ya mti mithili ya chemchem.
Baadhi ya Wakazi wa mji huo inasemekana waligundua maajabu hayo kwenye mti huo na baada ya wakazi hao kuanza kujizolea pesa toka kwenye mti huo habari ghafla zilisambaa mkoani Ruvuma kuwa kuna mti una chemchem ya pesa.
Ilidaiwa kuwa wakazi hao walipokuwa wakipita chini ya mti huo waliona pesa zikitoka chini ya mti na pamoja na kustaajabishwa na tukio hilo wakazi hao waliamua kuzichukua pesa hizo.
Taarifa zaidi zilisema kwamba kwa muda wa siku mbili mfulululizo wakazi wa wilaya ya Songea waliendelea kuziokota pesa zilizokuwa zikitoka kwenye mti huo.
Pesa hizo inadaiwa zilikuwa zikitoka mithili ya chemchem zikiwa ni noti tofauti tofauti zikiwemo na noti za shilingi elfu kumi, tano na kadhalika.
Baadhi ya watoto waliowahi kuhojiwa na mwakilishi wetu wa nifahamishe kutoka eneo la tukio, watoto hao walidai kuwa walishajizolea pesa hizo na walizipeleka kwa wazazi wao nyumbani.
Walidai kuwa pesa hizo zilikuwa zikitoka chini ya ardhi na mamia ya watu toka sehemu mbalimbali za mkoani Ruvuma walikuwa wakizigombania kila zilipoanza kuchomoza.
Watu wazima waliohojiwa na Nifahamishe nao pia walithibitisha kujizolea noti hizo zilizodaiwa kutoka kwenye chemchem hiyo.
Kwa kuwa pesa pesa hizo zilikuwa zinatumia muda mrefu kutoka kwenye chemchem hiyo, maelfu ya watu kutoka wilaya tofauti wamekuwa wakiweka kambi eneo hilo kusubiria pesa hizo.
Tukio hilo limethibitishwa na polisi mkoani humo na walisema wanafanya uchunguzi wa kina kubaini kuwa pesa hizo zinakuwa zinatoka wapi.
source nifahamishe

