Mtaalamu wa Mapenzi Atamba Kulala na Wanaume 1,500

Wednesday, September 16, 2009 / Posted by ishak /

Mwanamke huyu wa nchini Uingereza anayejiita mwenyewe Mtaalamu wa mambo ya mapenzi, amefanya mapenzi na wanaume zaidi ya 1,500 walioenda kwake kutafuta ushauri wa kimapenzi.
Katika wateja wake zaidi ya 10,000 walioenda kwake kutafuta ushauri wa kimapenzi katika kipindi cha miaka 23, mwanamke huyu anayejitamba kuwa yeye ndio mtaalamu wa masuala ya kitandani, amefanya mapenzi na wanaume 1,500 kati yao.

Mare Simone mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa kitongoji cha Chelsea, jijini London amejiajiri mwenyewe na ana ofisi yake jijini humo akitoa ushauri wa mambo ya kimapenzi kwa wanawake na wanaume.

Baada ya kuachana na mumewe, Mare aliamua kuisomea rasmi taaluma hiyo ya mapenzi na kisha kufungua ofisi yake ambapo hadi sasa ametoa somo la mapenzi kwa zaidi ya wateja 10,000 waliofika kwenye ofisi yake katika kipindi cha miaka 23.

Mare amesema kuwa hadi sasa ameishafanya mapenzi na wanaume zaidi ya 1,500 katika wateja wake ambao miongoni mwao ni waume au wapenzi wa wanawake wengine.

Mare anasema kuwa hafikirii hata kidogo kuwa anafanya kosa lolote kinyume cha sheria kutembea na waume za watu.

"Najipatia kipato changu kwa kulala na waume au wapenzi wa wanawake wengine. Lakini mimi sifanyi ukahaba kwakuwa taaluma ya mapenzi inaruhusiwa kisheria na mapenzi yanafanyika katika mazingira ya tiba" alisema Mare.

"Watu wananilipa kwa ushauri ninaowalipa na kwa kutibu matatizo yao hawanilipi kwasababu ya ngono".

"Nasaidia kuimarisha na kubadilisha maisha ya kimapenzi ya maelfu ya wanaume na hivyo nakuwa nimesaidia kuimarisha maisha ya kimapenzi ya wake zao au wapenzi wao"

"Wanawake wengine wanabeba mimba za wanawake wengine kwasababu wanataka kuwasaidia wanawake wasio na uwezo wa kupata mimba. Hali hiyo ni sawa na mimi kwani nawasaidia watu kuwa na maisha mazuri ya kimapenzi".

Mare alielezea kuifurahia kazi yake na huwa na furaha zaidi wateja wake wanapoondoka kurudi majumbani mwao wakiwa na matumaini mapya kwenye maisha yao ya kimapenzi.

Mare kwa siku anatoa vipindi vitano vya masuala ya mapenzi na anasema wateja wake ni watu wa rika mbali mbali. "Wateja wangu ni watu wa rika zote, jinsia zote, maumbile tofauti na wafanyakazi wa vitengo tofauti tofauti".

"Wanaume mara nyingi hunifuata kwa sababu ya matatizo ya kutosimama vyema kwa uume na kufika kileleni mapema kabla ya wapenzi wao wakati wengine huambiwa waje wanione na wake zao kwakuwa hawawaridhishi kitandani".

"Kabla hawajaniona huwa wote wanapimwa magonjwa ya zinaa na lazima watumie kondomu iwapo nitalala nao" alisema Mare.

"Kwa wanawake mara nyingi hunifuata wakiwa na matatizo ya kutofika kileleni au wanapoona wapenzi wao hawajui jinsi ya kuwaridhisha kitandani".

"Huwa nawafundisha jinsi ya kujipa raha wao wenyewe na kuipenda miili yao" alimalizia Mare.

source.nifahmishe.com

0 comments:

Post a Comment