Wezi Kama Hawa Hawajawahi Kutokea

Wednesday, January 06, 2010 / Posted by ishak /


Polisi nchini Sweden wamewatia mbaroni wezi wa kimataifa ambao staili yao ya wizi haijawahi kutokea duniani.
Wezi hao wa nchini Sweden walikuwa wakiwasumbua wafanyabiashara wa maduka makubwa ya viatu nchini Sweden na nchini Denmark.

Kwa kuwa katika maduka ya viatu ya nchini Sweden viatu vya kushoto ndio huwekwa kwenye shoo za maduka, wezi hao walikuwa wakiiba kiatu kimoja kimoja cha kushoto nchini Sweden na kisha kwenda kuiba kiatu cha kulia nchini Denmark ambako maduka huviweka viatu vya kulia kwenye shoo za shelfu zao.

Kutokana na staili hiyo ya wizi walifanikiwa kupata pea kadhaa za viatu vya gharama ambavyo waliviuza kwa bei poa.

Wakati wanatiwa mbaroni walikutwa na viatu sita vya kushoto ambavyo pea zake huuzwa kwa dola 1,400.

Wezi hao walikuwa wakifanya wizi huo katika mji wa Malmo nchini Sweden na Copenhagen nchini Denmark.

Mji wa Malmo una maduka yapatayo 125 ya viatu na kutoka Malmo hadi Copenhagen ni mwendo wa dakika 30 tu kwa treni.



Mtumie Rafiki Yako
Comments Add your Comment

Mtoa Maoni: moms016 Wednesday, January 06, 2010 00:54:39

Ni kweli mwanadamu hashikiki "ukimzibia huku anatoboa kule" lkn ndio tunarejea palepale kuwa iwapo mpanga sheria ni mwanadamu basi na mvunjaji ni huyohuyo.
BHAI uko wapi? seria kata bele na juma..
UBUGUVU endelea tu na kuvaa mapira ya gari, muhimu ni ya kwako hujamuibia mtu!
KING anatambea pekupeku!
DECLAKERS anauliza viau ni kitu gani?
Sis MINA anavaa viatu kisha soksi! Kuna kazi!

source.nifahamishe

0 comments:

Post a Comment