Gazeti Lamuaibisha Rais wa Ufaransa

Monday, July 19, 2010 / Posted by ishak /


Gazeti moja nchini Ufaransa limeingia matatani baada ya kutengeneza picha na kuziweka kwenye ukurasa wake wa mbele zikimwonesha rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy akiwa jela kama shoga akiinamishwa kwenye machuma.
Gazeti la vichekesho la Le Monte la Ufaransa katika tokeo lake la mwezi wa saba limeingia matatani baada ya kutengeneza picha za kumuaibisha rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy.

Gazeti hilo ambalo lilitakiwa liwe sokoni hadi mwezi wa nane, litaondolewa toka madukani kesho kufuatia uamuzi wa mahakama.


Gazeti ambalo lina idadi kubwa ya wasomaji lilitengeneza picha ikimuonyesha Sarkozy akiwa jela akiwa hana nguo hata moja akiingiliwa kinyume cha maumbile na mfungwa mwingine.

Picha hizo za kutengeneza ziliambatana na kichwa cha habari "Sarkozy akiwa jela".

Sarkozy ambaye hivi sasa yupo kwenye misukosuko mikubwa ya kisiasa alifungua kesi mahakamani kulishitaki gazeti hilo.

Nayo mahakama mjini Paris ilitoa hukumu ya kesi hiyo katika kipindi kifupi sana ambapo iliamua picha hizo za Sarkozy zifutwe katika nakala mpya zitakazochapishwa au la itabidi walipe faini ya euro 100 kwa kila picha itakayoonekana.

Katika kuimaliza kesi hiyo, hakimu alitowa hukumu gazeti hilo kumpa fidia Sarkozy sawa na euro 1(moja).

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment