Mchungaji Atumia Pesa za Kanisa Kufanya Ukahaba

Saturday, February 27, 2010 / Posted by ishak /


Mchungaji mmoja nchini Hispania ametimuliwa baada ya kutumia pesa za kanisa kujitangaza kwenye internet kuwa yeye ni kahaba wa kiume na alizitumbua pesa zaidi za kanisa kwa kupiga simu za ngono na kutembelea tovuti za kulipia za video za ngono.

Skendo hilo kubwa la mchungaji wa makanisa mawili ya katoliki katika mji wa Toledo, mchungaji Samuel Martin Martin, 27, limetawala magazeti ya Hispania ambapo magazeti mengi yalichapisha tangazo la kutafuta wateja la mchungaji huyo kahaba.

Mchungaji Martin aliweka tangazo hilo likiambatana na picha yake akiwa amevaa chupi ya kahawia akisema kuwa yuko tayari kufanya mapenzi na mwanamke yoyote kwa malipo ya euro 120 kwa lisaa limoja.

"Niko tayari kwa mapenzi ya staili zote, napatikana masaa 24 ukitaka nyumbani kwako au hotelini. Hautazijutia pesa zako, nitakupa raha ambayo hujawahi kuipata", lilisema tangazo la mchungaji Martin.

Mchungaji huyo ambaye alijitambulisha online kwa jina la Hector alijitamba kuwa ana mzee mwenye urefu wa sentimeta 15 ambaye yuko tayari kutoa uroda na furaha.

Mchungaji Martin aliwaomba radhi waumini wa makanisa hayo akisema kuwa alizitumia vibaya pesa za michango ya kanisa.

Anatuhumiwa kutumia euro 17,000 kwenye mitandao ya simu za mambo ya ngono na tovuti za video za ngono.

Skendo la Martin limeibuka wakati kanisa katoliki nchini Hispania linapigania kuwavuta waumini makanisani kutokana na kupungua kwa idadi ya watu wanaoenda makanisani.

Mchungaji Martin ametoweka tangia skendo hilo lilipoibuliwa magazetini na ameahidi kuzirudisha pesa alizoziiba kwenye michango ya kanisani


source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment