Msikiti waanguka na kujeruhi 50

Sunday, February 21, 2010 / Posted by ishak /


WATU zaidi ya 50 wamejeruhiwa vibaya baada ya msikiti kuanguka nchini Morocco siku ya Ijumaa walipokuwa wakijiandaa na sara ya Ijumaa.
Kuta za msikuti huo uliojengwa katika karne ya 16 uliopo kaskazini mwa mji wa Meknes ulianguka wakati waumini hao walipokuwa wakijiandaa kuanza swala.
Msemaji wa mamlaka ya mji huo Al-Elwi al-Ismaili amesema uokoaji bado uandelea ambapo majeruhi wote walikimbizwa hospitali ya karibu ya Bab Baradein.
Mapema kituo cha Pan-Arab al-Jazeera kiliripoti kuwa watu saba wamefariki dunia na 47 kujeruhiwa vibaya katika tukio hilo.

source gblp

0 comments:

Post a Comment