Sinema ya Ngono za Mashoga Yaonyeshwa Kanisani

Monday, February 22, 2010 / Posted by ishak /


Mchungaji wa nchini Uganda anayepigania sheria kali zipitishwe dhidi ya mashoga nchini humo, amewaonyesha waumini wake kanisani sinema ya ngono wanaume wakiwaingilia kinyume cha maumbile wanaume wenzao.
Waumini zaidi ya 300 waliojazana kwenye kanisa la mchungaji Martin Ssempa la mjini Kampala nchini Uganda, walishuhudia sinema ya ngono kanisani wanaume wakiwainamisha na kuwaingilia kinyume cha maumbile wanaume wenzao.

"Angalia mwanaume huyu anakula uume wa mwanaume mwenzake", alisema mchungaji Ssempa akitoa maelezo juu ya kipengele kimoja cha video hiyo.

"Je ni haya kweli Obama anataka kutuletea barani Afrika?", alisema mchungaji huyo kufuatia kauli ya Obama kupinga sheria kali dhidi ya mashoga nchini Uganda na kutaka mashoga nao wapewe haki zao.

Mchungaji huyo aliamua kuionyesha sinema hiyo kanisani katika kutafuta kuungwa mkono juhudi zake za kutaka sheria kali dhidi ya mashoga nchini Uganda.

Sinema hiyo ilionyeshwa siku ya jumatano na kuangaliwa na waumini wengi baada ya polisi nchini Uganda kuyafuta maandamano ya watu milioni moja yaliyokuwa yafanyike kuuunga mkono muswada wa kuwahukumu kifungo cha maisha mashoga.

"Tulikuwa tumepanga wanaume na wanawake milioni moja tuandamane kwenye jiji la Kampala lakini tuliambiwa kuwa hatuwezi kuandamana kutokana na sababu za kiusalama", mchungaji Ssempa aliwaambia waumini wake.

"Hivi mnajua ni vitu gani wanavyofanya mashoga wanapokuwa kwenye vyumba vyao?", alisema mchungaji huyo na kuanza kuwaonyesha waumini wake picha za ngono za mashoga.

Mchungaji huyo aliweka video ya picha zinazoonyesha wazi wazi jinsi wanaume wanavyowaingilia wanaume wenzao.

Serikali ya Uganda imekuwa ikipata upinzani mkubwa toka nchi wafadhili ambazo baadhi zimetishia kusitisha misaada yake iwapo Uganda itapitisha muswada wake wa kuwabana mashoga na wasagaji.

Katika mojawapo ya vipengele vya muswada huo, watu wanaowakodisha nyumba mashoga na wasagaji nao pia watakumbana na sheria na watafikishwa mahakamani.

Baadhi ya mashoga watahukumiwa adhabu ya kifungo cha maisha cha maisha na wengine adhabu ya kifo kama muswada huo utapitishwa.

source nifahamishe

0 comments:

Post a Comment