Mambo ya wachina

Sunday, February 21, 2010 / Posted by ishak /


Polisi wa Jimbo la Xinhua nchini China, wamelazimika kumpigia magoti mwanamke mmoja wakimuomba kufuta uamuzi wake wa kujirusha kutoka juu ya nyumba yenye urefu wa ghorofa saba, kufuatia mzozo aliotokea nyumbani kwake baina yake na mumewe.Kwa mujibu wa habari kutoka jimboni humo, mwanamama huyo Chan Bao, aliamua kuchukua uamuzi huo wa kupanda juu ya ghorofa ili kujitupa chini, kufuatia mumewe Cheng Dong kuondoka nyumbani kimya kimya bila ya kumtakia ‘Birthday njema’ wakati akijua fika kuwa siku hiyo ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa.

Kitendo cha mumewe kuondoka kimya kimya hakikumpendeza Chan, hali iliyomfanya ahisi amedharauliwa, jambo lilompandisha hasira na kufikia uamuzi wa kutaka kujirusha kutoka juu ya ghorofa. Hata hivyo dhamira ya mwanamke huyo haikutimia kwani baada ya polisi kuona haelewi, waliamua kumfuata hukohuko juu na kumteremsha chini kwa nguvu.

source globalp

0 comments:

Post a Comment