BEBE COOL AVUNJWA MIGUU KWA RISASI

Sunday, January 31, 2010 / Posted by ishak /



Mwanamuziki mashuhuri wa reggae nchini Uganda, Bebe Cool a.k.a Moses Sali, akiingizwa katika hospitali ya Nsambya jijini Kampala baada ya kupigwa risasi katika klabu moja jijini humo.

Kwa mujibu wa mtandao wa gazeti la The Monitor toleo la mchana huu, risasi hizo zimevunja miguu yote miwili, amesema Daktari Mratibu wa hospitali hiyo, Dk. Martin Nsubuga.

Habari zinasema risasi zilirindima katika klabu ya Effendys katika maeneo ya Centenary Park, na kwamba kuna utata wa sababu zilizopelekea purukushani hilo. Inasemekana watu wengine watatu ikiwa ni pamoja na mabaunsa wa Bebe Cool na askari wa kikosi maalum pia walijeruhiwa.

source globalpublisher

0 comments:

Post a Comment